Wilaya ya Sengerema imeanza kutekeleza kwa vitendo agizo la
Rais, baada ya kukamata watu wanane waliokutwa wakinywa pombe saa za kazi.
Amri ya kukamatwa na kuwekwa
mahabusu kwa watu hao ilitolewa juzi na Mkuu wa Wilaya Zainabu Terack, baada ya
kukuta baa zimefunguliwa asubuhi zikiwa na wateja waliokuwa wakipata kinywaji
kabla ya saa 9:30 alasiri, muda ambao ofisi za Serikali hufungwa.
Rais John Magufuli alitoa agizo
hilo la kupiga marufuku unywaji pombe na uchezaji pool nyakati za kazi, wakati
alipokuwa akiwaapisha wakuu wa mikoa mwezi uliopita.
Kwa mujibu wa mkuu huyo wa wilaya aliyeongoza oparesheni ya
dakika 45 ya kusaka wanaokunywa pombe na kucheza pool muda wa kazi, watuhumiwa
hao watafikishwa mahakamani kwa makosa ya uzembe na kukiuka amri halali ya
serikali.
Wakijitetea baada ya kutiwa
mbaroni baadhi ya waliokamatwa, walidai kuwa walienda baa kujiliwaza wakati wa
msiba wa ndugu yao waliyemtaja kwa jina la Petro Shoyo, na kumwomba mkuu wa
wilaya kuwasamehe kwa sababu ni kosa lao la kwanza.
Lakini mkuu huyo wa wilaya
alisisitiza wapelekwe mahakamani.
0 comments:
Post a Comment