Dawa inayotumika kwa matibabu ya kawaida, huenda ikategua kitendawili cha
kurefusha maisha na kuzuia uzee.
Hii ni kwa mujibu wa utafiti
mpya, ambao ulibainisha kwamba viwango vya chini vya dawa aina ya Lithium
vilisaidia kurefusha maisha ya nzi waliowekwa kwenye maabara.
Wanasayansi wamesema utafiti
huu unatoa matumaini ya kutoa dawa, kuwasaidia watu kuishi maisha marefu na
yenye afya.
Lithium inatumika katika
matibabu ya matatizo ya akili,kama mfadhaiko, na kusongwa na mawazo.
Hata hivyo ina madhara makubwa
ikiwa itatumika kwa viwango vya juu.
Haijulikani jinsi Lithium
inavyotibu matatizo ya akili, lakini alipopewa nzi dawa hiyo ilisaidia
kurefusha maisha yao.
Hata hivyo watafiti
wamesisitiza lazima dawa hii kutumiwa kwa viwango vya chini zaidi, kwani
viwango vya juu vinaweza kuleta maafa.
Kando na matatizo ya akili
Lithium imetumika kutibu maumivu makali ya kichwa 'Migraines' na ugonjwa wa
jongo unaomfanya mtu kuvimba viungo hasa wakati wa baridi.
0 comments:
Post a Comment