Mkuu wa Mkoa wa Arusha Felix Ntibenda, amepiga
marufuku uuzwaji wa kilevi aina ya kiroba katika mkoa wake.
Amesema uamuzi huo unatokana
na vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa, kushindwa kufanya kazi na kulewa wakati
wa kazi.
Aidha mkuu huyo wa mkoa amesema
anafanyia kazi sakata la mkazi wa Kata ya Ngarenaro anayedaiwa kujihusisha na
uuzaji na uingizaji wa dawa za kulevya, ambaye baada ya kukamatwa na polisi
aliachwa katika mazingira ya kutatanisha.
Ntibenda amesema hayo jana
Arusha wakati akizungumza na watendaji wa serikali za mitaa, maofisa watendaji
kata pamoja na wenyeviti wa serikali za mitaa.
Amesema suala la kilevi aina ya kiroba ni kero kwa
vijana kufanya kazi wakiwa wamelewa, au kuwa navyo mifukoni hasa madereva wa
pikipiki, daladala na wapiga debe.
Amesema kutokana na vijana
kunywa kinywaji hicho nyakati za kazi, amepiga marufuku uuzwaji wa kilevi
hicho, atakayekiuka agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa.
0 comments:
Post a Comment