Wanajeshi wa Korea Kusini wanasema kuwa,
Korea Kaskazini imefyatua kombora la
masafa marefu katika eneo la pwani ya
mashariki ndani ya bahari, wakati ambapo rais Barrack Obama anaongoza kikao cha
dunia kuhusu usalama wa Nyuklia mjini Washington.
Ufyatuaji
wa kombora hilo ni wa hivi karibuni, katika msururu wa ufyatuaji unaoendeshwa
na Pyongyang ambao umesababisha hali ya taharuki, baada ya taifa hilo
kutekeleza jaribio la zana za kinyuklia mwezi Januari.
Rais wa Marekani
Barrack Obama anasema China na Marekani, zitashirikiana kumaliza miradi ya
nyuklia ya Korea Kaskazini.
Bwana
Xi amezitaka pande mbali mbali kuidhinisha vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi
ya Korea Kaskazini.
0 comments:
Post a Comment