Imeelezwa kuwa watu elfu 1 mia 6 hasa watoto hufa nchini
kila mwaka, kutokana na ugonjwa wa
kichaa cha mbwa.
Hayo yalielezwa jana na Katibu
Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Mary Mashingo.
Dk Mashingo amesema vifo hivyo
hutokana na wagonjwa hao hasa watoto kukosa chanjo kwa wakati.
Na hiyo ni kutokana na kuwepo kwa
vituo saba pekee hapa nchini,ambavyo
vinatoa huduma hizo.
Ameitaja mikoa ambayo vituo hivyo
vipo kuwa ni Dar es Salaam, Tabora, Mwanza na Mikoa ya Kusini.
0 comments:
Post a Comment