Friday 29 April 2016

ASHINDA TUZO AKIWA MAHABUSU…..!!

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THDRC), umempa tuzo ya mwaka George Mgoba aliye mahabusu akikabiliwa na
shtaka la kuandaa kinyume cha sheria maandamano ya vijana, waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kushinikiza kupatiwa ajira.

Mgoba amepata tuzo hiyo ya mwaka kutokana na juhudi alizozifanya 2015 za kuwatetea vijana waliokuwa wanataka kuandamana, kushinikiza Serikali kutoa ajira kwa vijana waliomaliza mafunzo hayo.
Mkurugenzi wa THDRC Onesmo Ole Ngurumwa, amesema suala la haki za binadamu linabaki pale pale bila ya kujali mhusika amefanya nini, na anastahili adhabu gani iwapo itathibitika ana hatia.
Amesema utatuzi wa tatizo la ukiukwaji wa sheria kama upo uangaliwe ni kwa kiasi gani unafanyika bila kuathiri maisha ya binadamu na kumuondolea thamani yake.
Kauli mbiu ya mwaka huu inasema Tuwalinde Watetezi wa Haki za Binadamu”, ndiyo maana tumeona ni fursa ya kumkumbuka Mgoba ambaye hadi sasa anaumwa na bado ni mahabusu kwa zaidi ya mwaka, kwa kuwa na alipata matatizo hayo akiwa anatetea haki za wengine na yake kama binadamu.


0 comments:

Post a Comment