Afisa
mkuu wa jeshi la Burundi ameuawa pamoja na mkewe, baada ya kushambuliwa na watu
wasiojulikana mjini Bujumbura.
Jenerali Athanase Kararuza na
mkewe wameuawa wakiwapeleka watoto wao shuleni, afisa mmoja wa usalama ambaye
hakutaka jina lake litajwe ameambia shirika la habari la AFP.
Wizara ya ulinzi imethibitisha
kifo chake.
Jenerali huyo ndiye afisa wa
karibuni zaidi wa jeshi kuuawa katika mji huo mkuu wa Burundi tangu kufanyika
kwa jaribio la kupindua serikali ya Rais Pierre Nkurunziza mwaka jana
0 comments:
Post a Comment