Mwanafunzi wa chuo kikuu raia wa Iraq katika jimbo la California nchini
Marekani, anasema kuwa
alitolewa kutoka kwenye ndege ya shirika la ndege la
Southwest baada ya kufanya mazungumzo kwa lugha ya kiarabu.
Shirika hilo la Southwest
lilisema kuwa mwanafunzi huyo aliondolewa kwenye ndegeni tarehe 9 mwezi Aprili
kabla ya ndege hiyo kupaa.
Bw Makhzoomi anasema alikuwa
akizungumza na mjomba wake kwa njia ya simu, kuhusu hotuba ya katibu mkuu wa
Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon.
Anasema kuwa mwanamke mmoja
kwenye ndege hiyo alimkodolea macho wakati alitamka jina Inshallah akimaanisha
Mungu akipenda.
Baada ya kutumia jina hili
mfanyikazi wa shirika la Southwest alimtoa na kumsindikiza nje ya ndege hiyo..
Bw Makh zoomi ambaye aliingia
nchini Marekani kama mkimbizi kutoka Iraq na sasa ni mwanafunzi wa chuo kimoja
cha Carlifonia, amesema kuwa hawezi kuingia tena kwenye ndege hiyo.
0 comments:
Post a Comment