Polisi nchini Australia wamemshtaki mvulana mwenye umri
wa miaka 16, ambaye anasemekana
alikuwa akipanga kutekeleza shambulio katika
siku kuu ya wanajeshi wastaafu wa nchi hiyo.
Mvulana huyo alitiwa mbaroni
nyumbani kwake huko Sydney, alipodaiwa kupanga kutekeleza uhalifu huo wa
kigaidi leo Jumatatu wakati wa sherehe za siku kuu ya ANZAC, ya maadhimisho
hayo ya kuwakumbuka wanajeshi waliouawa vitani Australia.
0 comments:
Post a Comment