Serikali ya Canada itabuni sheria mpya
mwaka ujao, ambazo zitahalalisha uuzaji wa bangi.
Iwapo
sheria hiyo itaidhinishwa italiorodhesha taifa la Canada, miongoni mwa mataifa
yenye uchumi mkubwa magharibi kukubali matumizi wa bangi.
Waziri
mkuu Justin Trudeau alipigania dawa hiyo kuhalalishwa, wakati wa kampeni.
Waziri wake wa afya
amesema kuwa anataka dawa hiyo kutowafikia watoto pamoja na wahalifu.
Serikali
imeahidi kufanya kazi na maafisa wa polisi, ili kuwadhibiti wale wanaouziwa
dawa hiyo, wakati inapouzwa na vile inavyotumiwa na wametafuta njia ya
kudhibiti dawa hiyo kupitia sheria za uuzaji wa pombe.
Hatahivyo
wapinzani wanasema kuwa hatua mbaya zaidi kwa vijana, ni kuruhusu utumiaji wa
dawa hiyo ya kulevya.
Utumizi
wa bangi nchini humo utasalia kuwa marufuku, huku sheria za kuhalalisha
zikiendelea kutengenezwa.
0 comments:
Post a Comment