Shirika
la haki za kibibaadamu la Amnesty International limesema kuwa, kumekuwa na ongezeko
kubwa la idadi ya watu walionyongwa ulimwenguni mwaka uliopita, ikilinganishwa
na kipindi chochote tangu mwaka 1989.
Takriban watu elfu 1 mia 6 na 34 walinyongwa mwaka
2015,ikiwa ni ongezeko la asilimia 50 ikilinganishwa na mwaka wa 2014.
Imeelezwa kuwa nchi za Iran, Pakistan
na Saudia Arabia, walihusika na asilimia 89 ya watu wote walionyongwa duniani.
Jumla hiyo haishirikishi China ambapo Amnesty
International imesema kuwa,maelfu zaidi waliuawa lakini rekodi zake zikafichwa.
Kwa upande mwengine kundi hilo
limesema kuwa kwa mara ya kwanza, mataifa mengi duniani yalifutilia mbali
hukumu ya kunyonga.
Mataifa ya Fiji, Madagascar,Congo
Brazaville na Suriname, yalibadilisha sheria zao mwaka 2015, huku Mongolia
ikipitisha sheria mpya itakayoanza kutekelezwa baadaye mwaka huu.
Amnesty International imesema kuwa
China bado inaongoza miongoni mwa mataifa yanayonyonga watu.
Inakadiriwa
kwamba maelfu ya watu walinyongwa,huku maelfu ya wengine wakipewa hukumu ya
kunyongwa mwaka 2015.
0 comments:
Post a Comment