Friday 22 April 2016

UTAFITI:MILIONI 2.3 YA NGUVU KAZI NCHINI HAINA AJIRA…

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema kuwa,watanzania milioni 2.3 kati ya watu milioni 22.3 ambao ndio nguvu kazi ya taifa hawana ajira.

Kiwango hicho cha ukosefu wa ajira kwa mujibu wa NBS,ni sawa na asilimia 10.3 ya nguvu kazi ya taifa.
Kiwango hicho kinaelezwa kuwa kimepungua kutoka asilimia 11.7 ya mwaka 2006.
Hata hivyo utafiti huo umebainisha kuwa watu ambao hawana ajira, wamebainika wanatumia muda mrefu zaidi kusaka ajira.
Kwenye utafiti huo imebainishwa kuwa kiwango cha ukosefu wa ajira kwa muda mrefu, kimeongezeka kutoka asilimia 17.9 mwaka 2006 hadi asilimia 32.5 mwaka 2014.
Utafiti huo pia unaonyesha kuwa wanawake ndio kundi kubwa la Watanzania ambao wana kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira kuliko wanaume.
Pia utafiti huo unaonyesha kuwa asilimia 17.2 ya watu ambao wana uwezo wa kufanya kazi, hawana kazi na wala hawako tayari kufanya kazi yoyote ya kiuchumi.

Katika kundi hilo wamo wanawake ambao wengi wao wanajishughulisha na shughuli za nyumbani.

0 comments:

Post a Comment