Mvulana
wa umri wa miaka miwili amempiga risasi na kumuua mamake kimakosa, katika mji
wa Milwaukee nchini Marekani.
Mtoto huyo alipata bunduki hiyo
sehemu ya nyuma ya gari.
Mwanamke huyo Patrice Price 26
alikuwa akiendesha gari la mpenzi wake ambaye ni mlinzi, ambaye alikuwa ameacha
bunduki yake kwenye gari.
Polisi wa Milwaukee wanasema mwanamke huyo alipigwa
risasi moja kutoka nyuma,alipokuwa akiendesha gari mapema Jumanne asubuhi.
Mamake Price na mwanawe mwingine
wa kiume mwenye umri wa mwaka mmoja, walikuwa kwenye gari hilo wakati wa
kutokea kwa kisa hicho.
Bw Price alisema ana binti
mwingine mkubwa, lakini akasema Patrice alikuwa na bidii sana.
Mwezi uliopita mvulana wa umri wa
miaka minne alimpiga risasi mamake Jamie Gilt, katika jimbo la Florida katika tukio
linalofanana na hilo, lakini Bi Gilt alinusurika kwa kupata majeraha.
0 comments:
Post a Comment