Bunge
la Ufaransa limeidhinisha sheria mpya, inayopinga biashara ngono nchini humo.
Hatua hiyo inadaiwa kwamba huenda
ikaathiri maisha ya watu zaidi ya elfu thelathini, ambao wanategemea shughuli
za ngono katika kujipatia kipato ambao wengi wao ni raia wa kigeni.
Chini ya sheria hiyo mpya watu
watakaokutwa wakilipia huduma hiyo, wataadhibiwa kwa kulipa dola 1700.
Mmoja wa mbunge anayeunga mkono
sheria hiyo, ameitetea na kusema kuwa inalengo la kuhamasisha watu kujiondoa
katika biashara hiyo.
Hata hivyo kundi dogo la makahaba
waliandamana nje ya bunge, wakipinga sheria hiyo kwa madai kuwa wapewe uhuru wa
kujilinda wenyewe, na si kukatazwa kufanya biashara hiyo.
0 comments:
Post a Comment