Thursday 7 April 2016

BIASHARA YA UKAHABA YAPIGWA STOP UFARANSA.!

Bunge la Ufaransa limeidhinisha sheria mpya, inayopinga biashara ngono nchini humo.

Hatua hiyo inadaiwa kwamba huenda ikaathiri maisha ya watu zaidi ya elfu thelathini, ambao wanategemea shughuli za ngono katika kujipatia kipato ambao wengi wao ni raia wa kigeni.
Chini ya sheria hiyo mpya watu watakaokutwa wakilipia huduma hiyo, wataadhibiwa kwa kulipa dola 1700.
Mmoja wa mbunge anayeunga mkono sheria hiyo, ameitetea na kusema kuwa inalengo la kuhamasisha watu kujiondoa katika biashara hiyo.

Hata hivyo kundi dogo la makahaba waliandamana nje ya bunge, wakipinga sheria hiyo kwa madai kuwa wapewe uhuru wa kujilinda wenyewe, na si kukatazwa kufanya biashara hiyo.

0 comments:

Post a Comment