Monday 18 April 2016

IMARATI KUJENGA KITUO CHAKE CHA KIJESHI NJE YA NCHI…

Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) umeanza kujenga kituo chake cha kwanza cha kijeshi nje ya nchi huko Eritrea.

Taarifa zinasema kuwa picha za satalaiti zilizopatikana, zinaashiria kuwepo kituo kimoja kipya cha kijeshi na vile vile kuendelea ujenzi wa bandari katika uwanja wa ndege wa Assab huko Eritrea.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo inaonekana kuwa Imarati hivi sasa inajenga bandari hiyo mpya, pembeni ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Assab huko Eritrea, ambayo inaweza kuwa kituo cha kudumu cha kijeshi cha nchi hiyo nje ya Imarati.

Picha hizo za satalaiti zinaonyesha kwenda kasi kwa ujenzi huo,ulioanza baada ya mwezi Septemba mwaka jana.


Eritrea ni nchi inayopatikana katika pwani ya bahari Nyekundu kaskazini mashariki mwa Afrika, huku lango la kistratejia la Babul Mandab likiwa njia ya mawasiliano ya baharini kati ya nchi hiyo na Yemen.

0 comments:

Post a Comment