Mwanamuziki mmoja kutoka Uingereza, ameahirisha tamasha lake la muziki
visiwa vya Caribbean baada ya mbwa wake kuugua.
Joss Stones alisema mbwa huyo
kwa jina Missy ni kama mtoto kwake.
Aliandika kwenye ukurasa wake
wa Facebook kwamba aliahirisha tamasha la Jumamosi Katika kisiwa cha Barbados
na Jumanne kisiwa cha Trinidad, baada ya mbwa wake kuanza kuvuja damu.
Amesema anajua uamuzi wake huo
unaonekana kama jambo la kushangaza, lakini kwake mbwa huyo ni kila kitu.
Amesema anatumai kufanya
onesho nchini Venezuela tarehe 21 Aprili, kama mambo yakiwa sawa.
Stone tayari ameandaa maonesho India, Nepal, Panama na Costa
Rica kama sehemu ya safari yake nchi mbalimbali duniani, kuitangaza albamu yake
ya saba kwa jina Water For The Soul.
0 comments:
Post a Comment