Serikali
ya Ujerumani imetoa msaada wa ndege maalumu aina ya “Husky A-1C Aircraft” kwa
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Malisili na Utalii kusaidia katika doria
za kupambana na ujangili katika Pori la Akiba la Selous.
Msaada
huo wenye thamani ya Euro 200,000 sawa na Sh milioni 498.2 umekabidhiwa kwa
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na Waziri wa
Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo wa Serikali ya Shirikisho la Ujerumani, Dk
Gerd Muller katika hafla fupi iliyofanyika Matambwe ndani ya Pori la Akiba la
Selous.
Hafla
hiyo ilihudhuriwa na maofisa wa Ubalozi wa Ujerumani nchini wakiongozwa na
Balozi Egon Konchanke, viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Maliasili na
Utalii, Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA) na mashirika ya Maendeleo ya
Kimataifa ya FZS, WWF, GIZ na KFW.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Profesa Maghembe alisema ndege hiyo itasaidia jitihada za
Serikali za kupambana na ujangili kwa kufanya doria katika anga ya Pori la
Akiba la Selous na kusaidia kutoa taarifa za kiuhalifu pale itakapobainika na
kuchukuliwa hatua stahiki za kukabiliana na uhalifu huo.
Kwa
upande wake Waziri wa Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo wa Ujerumani, Dk
Muller alimueleza Profesa Maghembe kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana
na Tanzania katika kuendeleza uhifadhi nchini.
0 comments:
Post a Comment