Leo April 7, 2016 ni siku
ya kumbukumbu ya miaka 44 ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar
Hayati Sheikh
Abeid Amani Karume ambaye alizaliwa mwaka 1905 na kufariki tarehe 7 Aprili 1972
kwa kupigwa risasi.
Mzee Karume aliongoza nchi
baada ya mapinduzi yaliyomwangusha Sultani, aliyekuwa akitawala Zanzibar hadi
mwanzoni mwa mwaka 1964.
Baada ya miezi mitatu
Zanzibar iliungana na Tanganyika iliyokuwa ikiongozwa na Mwalimu Nyerere.
Baada ya Muungano wa nchi
hizi mbili uliozaa Tanzania, Mzee Karume alikuwa Makamu wa Rais wa kwanza wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hayati Sheikh Abeid
Amani Karume aliuwawa kwa kupigwa risasi ndani ya ofisi za Makao Makuu ya CCM
Kisiwandui, Unguja, wakati akicheza bao na marafiki zake.
Sehemu hii imewekwa uzio
maalumu ili kupahifadhi kama kumbukumbu, kwani kila kitu kipo vile vile
kilivyokuwa siku hiyo tukio hilo la kuuwawa kwake lilipotokea.
0 comments:
Post a Comment