Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kwamba
serikali yake itatenga dola za Kimarekani 10 milioni za kusaidia wakulima wa
mirungi kwenye bajeti ya mwaka ujao wa kifedha.
Wakulima hao
wameathirika sana kufuatia hatua ya baadhi ya nchi za Ulaya kupiga marufuku
uuzaji wa mirungi, maarufu pia kama miraa, katika mataifa hayo.
Hutumiwa sana na
watu wa jamii ya Wasomali na hutegemewa sana na jamii zianzoishi katika maeneo
ya mashariki ya Mlima Kenya, miongoni mwa watu wa jamii ya Wameru.
Pesa hizo
zitatolewa kupitia Wizara ya Kilimo.
Rais Kenyatta
ametangaza hayo alipokuwa akitia saini mswada unaotambua mirungi kuwa mmea wa
kuzalishia taifa mapato kuwa sheria.
Sheria hiyo
itaifanya serikali kuweka mikakati ya kutangaza, kuzalisha na kusambaza na
kuuza zao hilo.
Rais Kenyatta
amesema kutaundwa pia jopo kazi la kuangazia changamoto zinazokabili sekta ya
ukuzaji wa mirungi ambayo itatoa mapendekezo kwa serikali.
0 comments:
Post a Comment