Maelfu ya waandamanaji wamesafirishwa kwa mabasi hadi
katika mji mkuu wa jimbo la North Carolina nchini Marekani ili kufanya
maandamano.
Waandamanaji hao wameenda ili kuunga mkono na wengine kupinga
sheria mpya ya kitaifa, ambayo inawapa masharti makali watu wa mapenzi ya
jinsia moja (mashoga).
Sheria hiyo inasema kuwa watu
wanatakiwa kutumia vyoo vya umma, ambavyo vinashabiana na hali yao ya kijinsia
ya kuzaliwa sawa na inavyoorodheshwa katika cheti cha kuzaliwa, badala ya namna
wanavyojitambua kijinsia.
Sheria hiyo inawalengo wanaume mashoga wanaojisaidia katika
vyoo vya umma vya kike, kwa kile wanachosema kuwa wanajitambua kijinsia wao ni
wa kike.
0 comments:
Post a Comment