Kampuni ya
magari ya Volkswagen, imetangaza kuyanunua magari ya kampuni yake kutoka kwa
wateja nchini Marekani yapatayo nusu milioni.
Jaji kutoka San Francisco hajabainisha wazi kiasi ambacho
wamiliki wa magari hayo watalipwa na kampuni ya Volkswagen pale watakapo iuzia
kampuni hiyo magari yake wanayoyamiliki.
Makubaliano mengine yaliyofikiwa ni kwamba Volkswagen
itatakiwa kutoa fungu la fedha ili kuhamasisha tekinolojia ya kijani.
Wakili anayeiwakilisha kampuni ya Volkswagen Robert
Giuffra,amesema kampuni hiyo imekuwa ikifanya jitihada zote kuhakikisha
inapunguza uchafuzi wa hewa.
Upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili David Boies umesema
unataraji haki itatendeka kwa wamiliki wa magari hayo.
Katika hatua
nyingine maafisa kutoka taasisi ya kuzuia udanganyifu wa kifedha, kutoka
ufaransa wamezivamia ofisi za Peugeot citroen ,ikiwa ni muendelezo wa uchunguza
dhidi ya uchafuzi wa hewa kutokana na magari.
Msemaji wa kampuni hiyo anasema wameonyesha ushirikiano wa
kutosha katika kuchunguzwa kwao .
0 comments:
Post a Comment