Picha
ya mtumwa mmoja aliyekata nyororo na kisha kusaidia mamia ya wenzake kutoroka
utumwa, sasa itatumika katika noti mpya ya dola 20 nchini Marekani.
Bi Harriet Tubman atakuwa
Mwafrika Mmarekani wa kwanza, kuingizwa kwenye sarafu ya Marekani.
Vilevile ndiye mwanamke wa kwanza
katika kipindi cha karne moja, katika historia ya Marekani picha yakwe kuwekwa
kwenye dola.
Picha hiyo itabadilishwa na ile
ya awali ya rais wa saba wa Marekani Andrew Jackson, ambaye alikuwa akimiliki
watumwa enzi hizo.
Sasa picha ya Andrew Jackson
itakuwa nyuma ya noti hiyo.
Noti hiyo itaanza kutumika mwaka
2020 lakini idara ya fedha nchini Marekani, imesema ni mwanzo wa kuwakumbuka na
kuwaenzi waliopigania haki za kibinadamu nchini humo.
Bi Tubman alizaliwa miaka ya 1800
utumwani jimbo la Maryland na alifariki 10 Machi, 1913 akiwa eneo la Auburn
jimbo la New York.
0 comments:
Post a Comment