Watu wa jamii ya wafugaji wamepigwa marufuku, kwenda
na silaha za jadi katika sherehe mbalimbali hasa za harusi.
Amri
hiyo imetolewa na uongozi wa serikali ya kijiji cha Ntatumbila wilayani Nkasi
Rukwa, kutokana na silaha hizo kuhatarisha usalama.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Ignas Kanjele, amepiga
marufuku hiyo katika mkutano wa kijiji uliofanyika jana.
Amesema
katika kijiji hicho kumekuwa na tabia ya muda mrefu kwa wafugaji kutembea
wakimwa na sime, mikuki, mapanga na marungu, hali inayosababisha hofu kwa
baadhi ya wananchi kwa kuwa hawajui usalama wao.
Mwenyekiti huyo wa ulinzi na usalama wa kijiji hicho,
amesema kutokana na watu hao kutembea na silaha, baadhi yao wamekuwa wakiwapiga
wananchi na hata kuwajeruhi, hali ambayo amesema haivumiliki kijijini hapo.
0 comments:
Post a Comment