Watu wawili wameaga dunia baada ya
kuangukiwa na kifusi kwenye machimbo haramu ya dhahabu hapo juzi huko katika
mkoa wa Geita.
Kamanda wa polisi wa mkoa huo Mponjoli
Mwabulambo amethibitisha kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya alasiri juzi
Jumamosi, wakati watu watano walipokuwa ndani ya machimbo hayo yanayopatikana
katika kijiji cha Busaka katika wilaya ya Chato.
Kamanda Mwabulambo ameongeza kuwa mvua
zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya kanda ya ziwa yamedhoofisha kuta za
machimbo hayo ya madini na hivyo kusababisha kuporomoka.
Shaaban Ntarambe Mkuu wa wilaya ya Chato
ametangaza kufungwa eneo la machimbo hayo. Itafahamika kuwa Geita ni kitovu cha
uchimbaji wa madini ya dhahabu nchini Tanzania.
0 comments:
Post a Comment