Raia wa Tanzania Jemes Mwesiga (27)
aliyejiunga na kundi la al Shabaab la nchini Somalia, amenyongwa na kundi hilo
kwa tuhuma za ujasusi.
Mtandao wa habari wa Hiiraan Online
umeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, hukumu ya kifo dhidi ya Issa Jemes
Mwesiga (27) aliyejiunga na kundi la Al Shabaab mwaka 2013 ilitekelezwa na
kundi hilo siku ya Jumamosi.
Kwa mujibu wa mtandao huo jaji wa
mahakama hiyo alisoma hukumu hiyo mbele ya kadamnasi ya watu, kabla ya
kutekelezwa adhabu hiyo ya kifo katika uwanja ulio wazi.
Jaji huyo alidai kwenye hukumu yake
kwamba mtuhumiwa amekiri makosa kwa kuifanyia ujasusi Marekani, na hivyo
amehukumiwa adhabu ya kifo kwa kupigwa risasi.
Mpaka sasa serikali ya Tanzania
bado haijasema chochote kuhusiana na habari hiyo.
0 comments:
Post a Comment