Balozi wa Saudi
Arabia nchini Romania ambaye anakabiliwa na tuhuma ya kumbaka na kumuua
sekretari wake, amepewa masaa 48 afungashe virago na kuondoka nchini humo.
Mtandao mmoja wa
Habari nchini humo umeripoti kwamba, Abdulrahman bin Ibrahim alimbaka na kisha
kumuua sekretari wake ambaye ni raia wa Romania.
Wizara ya Mashauri
ya Kigeni ya Romania inamtuhumu balozi huyo kuwa, alimbaka Ivan Wilisco binti
wa Kiromania mwenye umri wa miaka 25 aliyekuwa akifanya kazi katika ubalozi huo,
kama sekretari wa balozi huyo.
Taarifa zaidi
zinasema kuwa uchunguzi wa kitiba uliofanywa unaonesha kwamba, binti huyo
alibakwa na kisha kunyongwa kwa kutumia mkanda.
0 comments:
Post a Comment