Je
ushawahi kugundua kuwa ukilala katika kitanda au mazingira mapya haupati
usingizi wa kutosha?
Sasa Utafiti umebaini kuwa mtu
akilala katika mazingira mapya ubongo wake haulali wote!
Upande wa kushoto wa ubongo huwa
uko chonjo dhidi ya hatari yeyote ile, hivyo haulali.
Utafiti huo wa chuo kikuu cha
Brown ulioongozwa na Profesa Yuka Sasaki, sasa umeanza kujaribu kutegua
kitendawili cha iwapo mtu anaweza kuzima upande wake wa kushoto wa ubongo
anapolala katika mazingira mapya?
Picha za ubongo wa watu
waliojitolea katika utafiti huu zinaonesha kuwa, upande huo wa kushoto huwa
ukitahadhari endapo patatokea sauti yeyote itakayoashiria hatari.
Utafiti huu ulithibitishwa
vilevile katika ndege na wanyama wengine
Utafiti mbadala katika chuo kikuu cha Rhode Island
umeonesha kuwa, ubongo wa binadamu unaweza kubadilika kadri inavyokabiliwa na
changamoto mpya.
Aidha Mtafiti huyo Sasaki anasema
kuwa, dhihirisho la hilo linapatikana kwa watu wanaosafiri kila kukicha.
0 comments:
Post a Comment