Wednesday 29 March 2017

RIPOTI YA FARU JOHN KUWANG’OA VIGOGO WAWILI…..

Kamati iliyoundwa kuchunguza utaratibu uliotumika kumhamisha Faru John kutoka hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyopo kwenye Hifadhi ya Grumeti Serengeti, imependekeza hatua za kinidhamu dhidi ya maofisa wawili wa Serikali waliohusika na uahamishwaji wa mnyama huyo.

Kamati haikufafanua aina ya hatua ambazo zinapaswa kuchukuliwa kwa maofisa hao, lakini imependekeza hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yao.
Aidha, Kamati hiyo imegundua kuwa Faru John alikufa kifo cha asili ambacho kilisababishwa na kutokupatiwa huduma za msingi za matibabu, ambapo imependekeza hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa wahusika kwa sababu hakukuwa na kibali rasmi cha kumhamisha kwenda mazingira ambayo yalisababisha kifo chake.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele alitoa mapendekezo hayo wakati akikabidhi ripoti hiyo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa juu ya uchunguzi walioufanya kuhusu uhamishwaji na kifo cha mnyama huyo.

Hata hivyo, Kamati hiyo imependekeza hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Profesa Alexander Songorwa na Daktari wa Shirika la Hifadhi la Taifa (Tanapa), Dkt. Moris Kileo.

0 comments:

Post a Comment