Saturday 11 March 2017

GARI LAANGUKA KATIKA PAA LA NYUMBA CHINA...

Gari moja lilipoteza mwelekeo katika mji wa Taizhou uliopo mashariki mwa China, kuteleza barabarani na kuanguka katika paa la nyumba.

Dereva wake alisema kuwa alijaribu kuzuia ajali ya ana kwa ana na bahati mbaya akakanyaga kichapuzi cha gari alipokuwa akibadilisha mwelekeo wa gari hilo.

Maafisa wa polisi walilazimika kutumia ngazi kumuokoa dereva huyo huku gari hilo aina ya SUV likiondolewa na korongo.

0 comments:

Post a Comment