Wednesday 29 March 2017

FIRST LADY WA ZAMANI WA IVORY COAST AACHIWA HURU….

Mahakama nchini Ivory Coast imemwachia huru first lady wa zamani Simone Gbagbo, aliyekuwa amefungwa kwa makosa dhidi ya ubinadamu.

Mashtaka yake yalihusiana na vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2010, pindi mume wake Laurent alipokataa kushindwa na Alassane Ouattara.
Majaji wengi wameyapinga mashtaka kuwa Simone Gbagbo 67 aliongoza machafuko hayo, na alijaribu kununua silaha.
First lady huyo alikuwa anatumikia kifungo cha miaka 20 kwa kuhatarisha usalama wa nchi.
Ivory Coast imekataa kumpeleka kwenye mahamakama ya kimataifa ya makosa ya jinai, ambako mume wake Laurent Gbagbo anashtakiwa kwa makosa dhidi ya ubinadamu.
ICC imetoa agizo la kukamatwa kwa Simone Gbagbo kwa makosa hayo pia.
Zaidi ya watu elfu 3 walipoteza maisha kwenye vurugu za uchaguzi nchini humo mwaka 2010.

Laurent na Simone Gbagbo walikamatwa mwaka 2011 baada ya wanajeshi kuvamia kificho walichokuwemo katika mji mkuu Abidjan.

0 comments:

Post a Comment