Monday, 29 February 2016

SAMATTA AIBEBA GENK…

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amefunga bao lake la kwanza
Ulaya wakati timu yake Genk ikichapa Club Brugge kwa mabao 3-2 katika Ligi Kuu Ubelgiji.
Samatta aliyeingia akitokea benchi katika dakika 77, alitumia dakika nne tu kupachika bao lake la kwanza na kuihakikishia timu yake pointi tatu muhimu kwenye Uwanja wake wa nyumbani wa Cristal Arena. Hicho ni kipigo cha kwanza kwa vinara wa Ligi Kuu Ubelgiji, Club Brugge mwaka huu.
Club Brugge ilianza mchezo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia Thomas Meunier, lakini Genk iliamka na kupata bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti dakika 36 mfungaji akiwa na Nikolaos Karelis, kabla ya Thomas Buffel kuongeza la pili dakika ya 50.
Samatta alipachika bao la tatu kwa wenyeji katika dakika ya 81, Club Brugge ilipata bao la pili kupitia Hans Vanaken katika dakika 83.


Hata hivyo, siku hiyo nzuri ya Samatta iliingia doa baada ya kuonyeshwa kadi njano katika dakika ya 90.

Related Posts:

  • STAILI YA UKAWA YABAMBA MITANDAONI…! Picha za watu wa kada mbalimbali nchini wakiigiza ‘staili’ mpya ya wabunge wa Ukawa waliojibandika karatasi midomoni zenye ujumbe tofauti kuhusu haki ya uhuru wa Bunge wanayodai kuminywa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson z… Read More
  • WATAOFANYA UASHERATI KUFUNGWA CAMEROON…!! Wanaume ambao hushiriki uasherati watafungwa jela, chini ya sheria mpya ambayo inajadiliwa na bunge la Cameroon. Mswada huo ambao ulipata uungwaji mkono wa chama cha Rais Paul Biya, unatarajiwa kuidhinishwa. Kwa s… Read More
  • BABA AJIWEKA TATOO KUFANANA NA MWANAWE ALIYEFANYIWA UPASUAJI… Baba wa miaka 28 nchini Marekani amenyoa kichwa chake na kuweka mchoro wa tattoo, unaofanana na kovu la kichwa cha mwanawe aliyefanyiwa upasuaji. Josh Marshall ambaye anatoka Kansas aliingia katika shindano la kila mw… Read More
  • SEKTA YA FILAMU ZA NGONO YAOMBA MSAMAHA JAPAN…! Muungano wa sekta ya filamu za ngono nchini Japan umeomba msamaha na kuahidi kuifanyia mabadiliko sekta hiyo kufuatia madai kwamba wanawake wanalazimishwa kufanya ngono katika filamu. Muungano wa kunadi picha hizo umese… Read More
  • TFDA YAKAMATA TENDE MPAKANI…! Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), imekamata tani laki sita za tende mpakani mwa Kenya na Tanzania, eneo la Hororo zilipokuwa zikiingizwa nchini kwa ajili ya kuanza kuuzwa. Mkurugenzi wa TFDA Thomas Nkoro am… Read More

0 comments:

Post a Comment