Wednesday 24 June 2015

Facebook kukutambua bila picha ya uso...!!!

Tayari mtandao huo wa kijamii wa Facebook unakusanya taarifa kutoka katika picha zako ili kubaini migao ya maoni kutoka kwa marafiki wako pale wanapoweka mtandaoni picha.

Sasa inaonekana mitandao ya kijamii inachukua mkondo mwingine wa kuboreshwa zaidi.
Watafiti kutoka katika idara ya upelelezi ya Facebook wamekuwa wakiifanyia kazi teknolojia hiyo mpya ambayo nia kuu ni kumtambua mtu hata kama uso wake hauonekani bayana kwenye picha.
Teknolojia hiyo iitwayo 'algorithm', inaangazia zaidi ya viungo mia moja vya mwanadamu.
Inatumika kwa pamoja katika kutambua uso wa mtu na pia mwili mzima wa binadamu.
Watafiti hao walitumia njia hiyo kwa kuzifanyia majaribio picha elfu 37 za watu ambazo zilitolewa kutoka kwa 'Flickr Commons'.
Wanasema kuwa njia hiyo ilitoa matokeo asilimia 83 ya watu 581 tofauti.

Matokeo hayo yaliwasilishwa mapema mwezi huu wa Juni katika kongamano la wakfu wa Computer Vision.

0 comments:

Post a Comment