Tuesday 16 June 2015

Askofu kushtakiwa kwa kudhulumu watoto…!!!

Askofu Josef Weslowski kushtakiwa kwa kudhulumu watoto

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, ameonekana kuanza kuwakabili makasisi waliotuhumiwa kwa sakata ya ngono.

Askofu mmoja aliyekua mjumbe wa papa katika jamhuri ya Dominican,atafikishwa mahakamani Julai 11.
Josef Weslowski raia wa Poland,ametuhumiwa kuwaharibu watoto wa kiume pamoja na kuwa na sinema chafu za watoto.
Kwingineko maaskofu wawili wa Marekani wamejiuzulu, kwa kukosa kuwalinda watoto ambao walidhulumiwa kimapenzi na makasisi.
Mwanadiplomasia huyo wa zamani amekuwa katika kifungo cha ndani huko Vatican, tangu alipovuliwa wadhfa aliokuwa amepewa na kurudishwa kutoka Jamhuri ya taifa la Dominican mwaka wa 2013.
Sasa atakabiliwa na kesi kwa mujibu wa sheria mpya zilizoidhinishwa na Papa Francis.
Hii inamaanisha kuwa anaweza kupewa kifungo cha hadi miaka 12 jela iwapo atapatikana na hatia .
Askofu mwengine wa kanisa la Mtakatifu Paulo huko Minnesota Marekani pamoja na msaidizi wake,nao walijiuzulu baada ya kushtakiwa kwamba walishindwa kuchukua hatua dhidi ya kasisi mmoja aliyeripotiwa kumnyanyasa mtoto kingono katika jimbo lake.
Papa Francis na viongozi waliomtangulia wamekuwa wakishtumiwa vikali kwa kukosa kuwachukulia hatua au hata kuwaondoa mamlakani,makasisi wanaoripotiwa kwenda kinyume na maadili na hasa unyanyasaji wa kingono .
Mapema mwezi huu Papa Francis aliunda tume maalum iliyopewa mamlaka ya kusikiliza na kuhukumu maaskofu wanaotuhumiwa kufumbia macho vitendo vya unyanyasaji wa kingono ambayo huenda vinaendelea katika makanisa yao.

Kwa namna hiyo inavyoelekea ni kwamba Papa Francis angependa mashtaka dhidi ya watumishi wa makanisani yashughulikiwe na mahakama maalum ya kanisa badala ya kesi hizo kupelekwa kwa mahakama za kawaida za umma.

0 comments:

Post a Comment