Wednesday 3 June 2015

Mkuu wa FIFA, Sepp Blatter ajiuzulu ghafla..!!!



 Rais wa Shirikisho la Soka Duniani  FIFA ametangaza kujiuzulu katika wadhifa wake huo siku chache tu baada ya kuchaguliwa kwa wingi wa kura kuliongoza shirikisho hilo.

Hatua hiyo ya Blatter imewashtua wengi kwani alikuwa amechaguliwa kuongoza shirika la soka la FIFA kwa muhula wa 5 Ijumaa tarehe 29 mwezi Mei.
Lakini kuchaguliwa kwake tena kuliongeza shinikizo kutoka kwa mashirika ya soka Ulaya na baadhi ya wadhamini waliomtaka ajiuzulu kama rais wa FIFA.
Katika kikao cha waandishi wa habari kilichoandaliwa ghafla hapo jana jioni, Blatter alitangaza kuwa ataondoka usukani katika miezi michache ijayo na akaitisha uchaguzi mpya wa kumchagua mrithi wake.
" Ikumbukwe kuwa punde baada ya kucaghuliwa Ijumaa iliyopita, Blatter alilaani vikali vyombo vya sheria vya Marekani kwa kuwashtaki maafisa wa shirikisho hilo kabla ya uchaguzi wa uongozi wake. Aidha aliwakosoa wakuu wa mashirikisho ya soka ya Ulaya kwa kuendesha kile alichokitaja kuwa ni 'kampeni ya chuki'.
Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Kongresi Marekani wanaishinikiza FIFA ibatilishe uamuzi wake wa kuipatia Russia haki ya kuandaa Kombe la Dunia mwaka 2018.
Blatter amesema Marekani imeanzisha uchunguzi dhidi ya FIFA baada ya nchi hiyo kunyimwa haki ya kuandaa Kombe la Dunia mwaka 2022.
Hivi karibuni pia Rais Vladimir Putin wa Russia alikosoa uchunguzi wa Marekani ndani ya FIFA na kusema, Washington inawashtaki kinyume cha sheria maafisa wa shirikisho hilo la soka duniani. Amesema huo ni mfano wa wazi wa kiburi na uingiliaji wa Marekani katika masuala yasiyoihusu.

0 comments:

Post a Comment