Tuesday 31 March 2015

Walimu witishia kugoma mkoani Kagera!!!

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Chama cha walimu wilaya ya MISENYI mkoani Kagera wanatarajia kuitisha mgomo usiokuwa na kikomo kwa kutofundisha katika shule za msingi na sekondari endapo uongozi wa halmashauri ya wilaya ya misenyi wataendelea kupoteza nyaraka zao mbalimbali zikiwemo za madai ya malipo na zile za kupandishwa madaraja.

Kwa mujibu wa taarifa lilyorushwa na ITV ni kwamba baada ya uchaguzi wa viongozi wa chama cha walimu wilaya ya misenyi,wamesema kuwa katika kikao cha utekelezaji CWT imeutaka uongozi wa halmashauri ya wilaya ya misenyi kutatua migogoro ya waimu katika kipindi cha wiki mbili na watakapokaidi chama cha walimu kitaitishwa mgomo kwa walimu wote wa shule za msingi na sekondari bila kujali kuwa wakati huu ni wakati wa kuandaa wanafunzi kufanya mitihani ya taifa.
 
Akijibu malalamiko hayo kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Misenyi Bw. Moses Gwaza amekanusha vikali tuhuma hizo na kusema kuwa katika kipindi cha miezi mitatu serikali imelipa madeni ya walimu katika wilaya ya Misenyi zaidi ya shilingi miioni 338 na kwamba walimu 96 madai yao hayapo kwenye bajeti ya mwaka huu na kuwataka kuwa na subira wakati serikali ikijipanga kuwalipa.
 

0 comments:

Post a Comment