Friday 20 March 2015

WhatsApp yasababisha mke kupewa talaka!!!

Mwanamume mmoja nchini Saudia amempa talaka mkewe kutokana na ujumbe wake katika mtandao wa WhatsApp.

Kulingana na gazeti moja la kiharibu Al Hayat, mwanamume huyo amedai kwamba mkewe aliandika ujumbe unaosema ''naomba kuwa na subra ya kutosha ili kuweza kuishi na wewe''.
''Nilimpigia mmoja ya ndugu zangu kumuuliza iwapo ujumbe ule ulikuwa unanilenga mimi'', alisema mwanamume huyo.
Watu wa Familia yangu walithibitisha hilo na nilisikia aibu kubwa kwamba mabibi za marafiki zangu pamoja na watu wa familia yangu wanaona ninaaibishwa.
Hata sielewi alikuwa akimaanisha nini''.Amesema kuwa ndo yake ilikuwa taabani na kwamba kitendo hicho hakikustahili kufanyika.Si mara ya kwanza amenichafulia jina katika mtandao wa kijamii.
Niliamua kumpa talaka kabla ya kuyatamgaza maisha yangu katika mitandao ya kijamii.'',
Khalid Al Habibi naibu mkurugenzi wa kituo cha kijamii kinachojihusisha na watoto mayatima anasema kuwa mitandao ya kijamii ni chanzo kikuu cha talaka.

0 comments:

Post a Comment