Wednesday 29 April 2015

Mawasiliano ya kijamii yakatwa Burundi…!!!

Utawala nchini Burundi umekata mawasiliano ya mitandao ya kijamii kupitia kwa simu za mkononi, mawasiliano ambayo wamekuwa wakitumia kupanga maandamano ya kumpinga rais Pierre Nkurunziza. Mamia ya waandamanaji wako barabarani kwenye mji mkuu wa Buruni,Bujumbura kwa siku ya nne ya ghasia kutokana na uamuzi wa rais kwa kuwania muhula wa tatu.

0 comments:

Post a Comment