Kiongozi wa Chama cha ACT, Zitto Kabwe
amesema zaidi ya Wabunge 50, watajiunga na chama hicho, Wizara ya
kilimo na chakula imewasimashisha kazi wakurugenzi watatu kwa kukutwa na
tuhuma mbalimbali,TAKUKURU imewataka wananchi kuwachagua viongozi
waadilifu wasiojihusisha na rushwa, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe amesema jamii za Afrika zinatakiwa kuwa kitu kimoja ili kuepuka machafuko yanayotokea.
Jeshi la Polisi limetoa onyo kwa wafuasi wanaotaka kumsindikiza Askofu Gwajima
kwenda kuhojiwa,TABOA imesema madereva waliopanga kugoma hawatambuliwi
kisheria, Serikali inatarajia kuzibana taasisi za kibiashara ili
kujiunga na soko la hisa ili ziweze kufanya shughuli zake kwa uwazi, na
wazazi wa Mtanzania, Rashid Charles Mberesero anaetuhumiwa kuhusika katika mauaji katika Chuo cha Garissa Kenya, wameelezea kushtushwa na taarifa za mtoto wao.
0 comments:
Post a Comment