Nimekutupia hapa kiduchuu tuu,habari ambazo zipo katika magazeti mengi ya leo April 14-2015
Miili 19 ya watu walioteketea kwa moto
katika ajali ya basi na lori Morogoro, imezikwa katika kaburi la pamoja
Kilosa, Wasomi na wanasiasa wamesema nchi inapita katika kipindi kigumu
kwa sasa kulingana na matukio mbalimbali yanayotokea, Serikali
imeshindwa kuweka wazi kufungwa kwa shule zake za sekondari kutokana na
ukosefu wa chakula, ndoa ya mwanamke mwenye miaka 54 na kijana wa miaka
25 yakwama Dar, Rais Kikwete amesema bado hajapelekewa majina ya watu 16 waliohukumiwa kifo kutokana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif jana
alifika mahakama ya Kisutu kusikiliza kesi ya wafuasi wa chama cha CUF,
Serikali imetangaza rasmi ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu Dar na meli
ya Mv Liemba kuwa sehemu ya urithi wa taifa, Jeshi la Polisi Katavi
linamshikilia mganga wa jadi kwa tuhuma za kukutwa na fuvu la kichwa cha
binadamu na BAWATA imepiga marufuku baadhi ya waganga wanaotoa huduma
kwenye nyumba za wageni.
0 comments:
Post a Comment