Thursday 9 April 2015

Obama apinga ubadilishaji wa maumbile.!!!!.




Rais Barrack Obama amesema swala la kisaikolojia miongoni mwa vijana ili kubadilisha maumbile yao linafaa kukoma mara moja.

Wengi wa wanaotaka kufanyia mabadiliko ya maumbile yao ni watu wa mapenzi ya jinsia moja hasa vijana.
Mshauri mkuu katika Ikulu ya Marekani Valerie Jarrett, amesema kuwa utawala wa Bwana Obama umekubali kwa kauli moja kuwa ushahidi wa kisayansi kuhusiana na maamuzi ya kujibadilisha maumbile, ni swala ambalo haliwezi kukubalika kitaaluma na kimatibabu.
Taarifa hiyo ya Obama inajiri baada ya kifo cha kijana mmoja ambaye alikuwa amebadili jinsia yake na ambaye alijitia kitanzi mwezi wa Disemba baada ya kulazimishwa kuhudhuria mabadiliko hayo ya kimaumbile.


0 comments:

Post a Comment