Wednesday 29 April 2015

Indonesia yawanyonga wauza mihadarati..

Indonesia imewaua wauzaji wanane wa mihadarati baada ya kutoa hukumu ya kifo dhidi yao.

Hukumu hiyo imetekelezwa na kikosi maalum cha kuwapiga wafungwa risasi, licha ya mwito kutoka kwa mataifa ya dunia ya kuwahurumia watu hao.
Kuuwawa kwa mfungwa wa tisa raia wa Ufilipino Mary Jane Veloso, kumecheleweshwa baada ya mwanamke mmoja kujiwasilisha kwa polisi Nchini Ufilipino, akisema kuwa ndiye aliyemhadaa mfungwa huyo mwanamke mwenzake, kupeleka dawa za kulevya hadi Indonesia

0 comments:

Post a Comment