Baada ya miezi kadha ya mizozo ya
kisiasa, rais wa Afghanistan Ashraf Ghani amewaapisha mawaziri 16 wapya
kwenye sherehe zilizofanyika mjini Kabul.
Hii inamaanisha kuwa baraza la mawaziri sasa limekamilika. Nafasi ya waziri wa ulinzi imesalia wazi kufuatia kutoelewana kwa serikali ya umoja.
Wale wote walioteuliwa hawajashikilia nyadhifa kama hizo na wengi ni vijana na waliosoma. Wanne kati ya mawaziri hao ni wanawake.
Kinyume na ilivyo kuwa awali, rais Ghani ameahidi kuwateua watu walio na ujuzi badala ya mibabe wa kivita na wapiganaji kuongoza serikali.
>>>>Bbc
0 comments:
Post a Comment