Wednesday 1 April 2015

Kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa yachafua Bunge!!!






Spika wa Bunge Anne Makinda katika kikao cha Bunge asubuhi ya leo, amelazimika kusitisha kikao cha bunge kwa muda usiojulikana,kufuatia
mtarafuku uliosababishwa na miongozo juu ya suala la kura ya maoni kwa katiba inayopendekezwa.
Mzozo ilianza pale mbunge wa Ubungo Mheshimiwa John Mnyika , kuomba mwongozo,akihitaji swala la kura ya maoni kujadiliwa leo hii kabla ya kutolewa majibu na serikali,kutokana na changamoto kadha wa kadha ambazo zimekuwa zikijitokeza katika zoezi zima la uandikishwaji katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Licha ya spika wa Bunge kutaka serikali ilitolee ufafanuzi suala hilo pindi waziri mkuu atakaposimama kuahirisha bunge,wabunge wa upinzani waliendelea kusimama na kushinikiza kutolewa kwa kauli ya serikali.
Hebu sikia hapa jinsi sinema hiyo ilivyokuwa huko bungeni mjini Dodoma.
Insert 1-Mzozo Bungeni

0 comments:

Post a Comment