Hii sio mbali sana, inatokea mtaa wa Old
Ngara, Kenya ambako kuna mzee mmoja ambae ameishi kwenye nyumba kwa
muda mrefu,zaidi inaweza kuwa rekodi mpya sababu sikuwahi kuisikia kwingine
.
Mzee huyo Adam Mamuji
amesema ameishi kwenye nyumba hiyo tangu mwaka 1944 kabla nchi hiyo
haijapata uhuru, wakati huo alikuwa akiishi na wazazi wake ambao
walifariki,kipindi hicho kodi ilikuwa shilingi 45 za Kenya.
Mzee Adam
amesema mwaka 1948 kodi ilipanda na kufikia shilingi 140, lakini kwa
sasa wanalipa shilingi elfu 10 za Kenya.
Amesema hawezi kutafuta nyumba
nyingine tena kwa sababu ameishi kwa muda mrefu kwenye nyumba hiyo
ameiomba Serikali imuuzie.
Nimeamini hakuna watu watunzaji wa vitu kama wazee, huyu mzee ametoa mpaka risiti ya Kodi ya nyumba aliyolipia miaka ya 1940 !!
Hii story yote nimekuwekea hapa chini kwenye video,ambayo iliripotiwa na kituo cha K24 Kenya.
0 comments:
Post a Comment