Katika
hatua ya kushitua Mahakama Kuu nchini Kenya, imesalimu amri mbele ya
mashinikizo ya watetezi wa vitendo vichafu vya ulawiti na usagaji,
na kusema
kuwa sasa watu wanaojihusisha na vitendo hivyo vya uasherati wanaweza kusajili
mashirika ya kile kinachodaiwa ni kutetea haki zao za kibinadamu.
Majaji
watatu wa mahakama hiyo wameiamuru Bodi ya Kusimamia Mashirika yasiyo ya
Kiserikali (NGOs), kulitambua na kulisajili shirika moja ambalo awali mahakama
hiyo ilizuia lisisajiliwe kwa sababu za kimaadili na kidini.
Jopo
hilo la majaji Isaac Lenaola, Mumbi Ngungi na George Odunga limedai kuwa,
katiba ndio marejeo ya kila kitu nchini Kenya na kwamba serikali haitakiwi
kuzingatia mafundisho ya kidini katika maamuzi yake ambayo kwa mujibu wa majaji
hao, maamuzi hayo yananyima kundi fulani la watu uhuru wao.
Hatua
ya Mahakama Kuu ya Kenya imechukuliwa pia katika wakati huu wa kukaribia ziara
ya Rais Barack Obama wa Marekani nchini Kenya, ambaye ni mtetezi mkuu wa
vitendo hivyo vichafu.
0 comments:
Post a Comment