Thursday 9 April 2015

Raia wa South Carolina waandamana kupinga ubaguzi..



Wakazi wa jimbo la South Carolina nchini Marekani waliandamana jana kulaani mauaji ya dereva mweusi aliyepigwa risasi na kuuawa na polisi mzungu.

Waandamanaji hao ambao wengi wao walikuwa Wamarekani wenye asili ya Afrika,wameonesha kusikitishwa na mauaji hayo ambayo wanasema yamefanyika kwa sababu za kibaguzi.
Dereva huyo alipigwa risasi na polisi barabarani baada ya kutokea mabishano baina ya wawili hao.
Mkanda wa video wa mauaji hayo unamuonesha polisi Michael Slager akimpiga risasi 8 mgongoni dereva huyo,huku akijaribu kukimbia.
Kesi ya Scott imezusha tena mjadala mkubwa nchini Marekani kuhusu mauaji yanayofanywa na polisi wazungu wa nchi hiyo dhidi ya raia weusi

0 comments:

Post a Comment