Tuesday 21 April 2015

Uharamia wapungua duniani

Maharamia
Halmashauri ya kimataiafa ya safari za baharini IBM imetoa ripoti yake ya hivi punde kuhusu uharamia.

Halmashauri hiyo inasema kuwa uharamia sasa unaripotiwa kusini mashariki mwa bara Asia, huku meli ndogo za kusafirisha mafuta zikishambuliwa baada ya kila wiki mbili.
Maeneo yaliyoathirika na uharamia
Kwenye ripoti yake ya kila baada ya miezi mitatu, IMB inasema kuwa licha ya kupungua kwa mashambulizi kote duniani miaka ya hivi majuzi, visa vya uharamia viliongezeka katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka 2015.
Ripoti hiyo inasema kuwa kwa mara ya kwanza hakuna visa vyovyote vya uharamia vilivyorekodiwa pwani ya Somalia na Ghuba ya Aden.
Inasema kuwa uharamia ulianza kushuhudiwa mwaka 2007 eneo hilo lakini ukapungua kuanzia mwaka 2011 wakati doria za meli za kijeshi zilipo ongezeka.
Ripoti hiyo pia imetaja visa kadha vya uharamia pwani ya magharibi mwa Afrika. Inasema kuwa mwaname moja aliuawa wakati wa kutekwa kwa mashua ya uvuvi pwani ya Ghana.

0 comments:

Post a Comment