Rais Jakaya Kikwete
ametoa msamaha kwa wafungwa 4,129 katika maadhimisho ya miaka 51 ya
Muungano, Mwalimu mkuu huko Lindi amekuta jeneza limewekwa mlango wake,
watu wanaozaniwa kuwa majambazi wamefukua kaburi huko Kibaha na kuiba
vitu alivyozikwa navyo marehemu, SUMATRA na Jeshi la Polisi kuanza
ukaguzi wa mikataba ya madereva wa mabasi na malori, wizara ya mambo ya
ndani inatarajia kufuta taasisi 24 kwa kushindwa kuwasilisha taarifa za
ukaguzi.
Mbunge wa Ubungo John Mnyika ambae
amemtaka Spika wa Bunge kuitisha kwa dharura kamati ya kudumu ya
katiba, sheria na utawala, Watanzania 26 wamerejea nchini kutoka Afrika
Kusini, waliokuwa wakimbizi zaidi ya 152 ,572 walioingia nchini mwaka
1972 wamekabidhiwa vyeti vya uraia wa Tanzania na ghasia zimeibuka
nchini Burundi kati ya maafisa wa Polisi na waandamanaji.
0 comments:
Post a Comment