Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Sekondari ya Matui iliyopo Wilayani Kiteto, Mkoani Manyara Emmanuel Mbigima mwenye miaka 15,amefariki dunia
baada ya kuchapwa viboko 12 na walimu wake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Christopher
Fulme,amesema mwanafunzi huyo alifariki dunia baada ya kuchapwa viboko
na walimu wake watatu kutokana na kufeli somo la Kiswahili.
Mauaji hayo yalitokea juzi saa 4 asubuhi shuleni
hapo na mwili wake kwa sasa unaendelea na uchunguzi.
Msemaji wa familia Emmanuel Ngowi,
amesema familia inataka kuona haki inatendeka juu ya kifo chandugu yao.
Chama cha Walimu Kiteto kimelaani tukio hilo na
kutaka uchunguzi wa kina ufanyike ili kujua ukweli kuhusu kifo cha mwanafunzi
huyo.
Hata hivyo baada ya taarifa hizo kuzagaa mitaani
kundi la wananchi wenye hasira kali walivamia kituo cha Polisi kwa lengo la
kulipiza kisasi kwa kutaka kuwaua walimu hao.
0 comments:
Post a Comment