Monday 20 April 2015

Ubalozi wajiandaa kuondoa Watanzania Afrika Kusini!!



 
Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini umesema umeanza utambuzi wa Watanzania waishio katikmaeneo ya hatari nchini humo,kabla ya kuanza hatua za kuwaondoa na kuwarejesha nyumbani.

Hatua hiyo inatokana na kushamiri kwa mashambulizi yanayofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya raia wa kigeni,ambapo hadi kufikia jana watu sita wameuawa.
Taarifa zilizopo hata hivyo zinasema kwamba hakuna raia wa Tanzania ambaye ameuawa au kujeruhiwa katika vurumai hizo ambazo zimeanza Durban, Kwa- Zulu Natal.
Mkuu wa Mawasiliano, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mindi Kasiga, amesema kwamba Ubalozi Afrika Kusini umepeleka maofisa wake katika mji wa Durban kuangalia hali ilivyo.
Kasiga amesema kwamba serikali imeshatoa mwongozo wa namna ya kuwaondoa raia wake nchini Afrika Kusini.
Amesema kwamba Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, ambaye yuko nje kwa safari ya kikazi atatoa taarifa mara tu atakapowasili nchini.

Kiwale 11 blog imezungumza na kaimu balozi wa Tanzania nchini humo Elibahati Lowassa, akieleza hali ilivyo mpaka sasa nchini humo,Bonyeza hapa chini kumsikia.




0 comments:

Post a Comment